Habari
Kituo cha polisi chashambuliwa mjini Mombasa, Kenya na polisi kadhaa kuuawa
Takriban polisi wanne mjini Mombasa, Kenya, waliokuwa wamesambazwa kuhakikisha amani kwenye uchaguzi wa urais unaofanyika leo wamevamiwa na kuuawa na kundi la watu saa chache kabla ya vituo vya kupigia kura kufunguliwa.
Kwa mujibu wa BBC washambuliaji waliokivamia kituo cha polisi mjini Mombasa wanashukiwa kuwa wafuasi wa kundi la Pwani la Mombasa Republican Army (MRC) ambao wamekuwa wakipigania uhuru wa jimbo la Pwani.
Hata hivyo shambulizi hilo huenda halihusiani na masuala ya uchaguzi.