Burudani
Lamar atayarisha wimbo wa kupiga vita dawa za kulevya uliofanywa na wasanii zaidi ya 10
Producer wa Fish Crub, Lamar ameproduce wimbo wa wasanii zaidi ya 10 wa Tanzania wenye lengo la kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya.
Amesema bado utengenezaji wa ngoma hiyo unaendelea na wasanii wengine wanaendelea kuingiza sauti zao.
“Wasanii waliofanya ni zaidi ya 10 sababu wanafanya bars nne nne, ina kama dakika 5 hivi,” Lamar aliiambia Bongo5.