Burudani

Maadui wa Afande Sele waitumia picha yake aliyovua suruali jukwaani kumchafua kisiasa

Internet ni maktaba kubwa ambayo maandishi, muziki, video na picha zikishasambaa huwezi kuvifuta daima. Na ndio maana picha maarufu ya mfalme wa rhymes Seleman Msindi aka Afande Sele inayomwonesha akirap jukwaani akiwa kifua wazi na kuvua suruali huku akibaki na ‘boxer’ nyeusi imeendelea kuwa jinamizi linalomrudia kila kukicha.

Na sasa kwakuwa rapper huyo aliyepotea kwenye playlist ya radio nyingi Tanzania ametangaza nia ya kugombea nafasi ya kubwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2015, amejikuta katika wakati mgumu baada ya maadui zake kutumia magazeti ya udaku kumchafua kwa kuitumia picha hiyo.

“Haya magazeti yanakwenda wapi?” alihoji Afande kupitia Clouds FM. “Katika furaha yangu, mimi siku hiyo ilikuwa ni siku ya birthday ya mtoto wangu Tunda nikaonesha na mimi bukta yangu ambayo ilikuwa na maandishi watu wakachukulia kama kawaida. Lakini sasa watu ambao hawakupendi ndio wanakuza lolote lionekane baya na sio ajabu, wiki moja baadaye 50 alikuja akavua akabaki na chupi. Mbona 50 kavua kabaki na chupi watu wanamshangilia?”

“Wanavyoenakana wametumwa. Sio siasa nzuri ni siasa chafu, mapema sana hatuwezi kuikomboa nchi kwa mazingira hayo. Pengine labda shida yao mimi nionekane mimi labda ni chizi au ni mwendawazimu kwahiyo yawekazana watanzania pia wameona sasa hivi wanahitaji viongozi wendawazimu kama sisi, kwasababu wameshaamini viongozi wenye akili mpaka leo ni nchi inayoongoza kwa umaskini duniani. Ina rasilimali kibao lakini hawa wanaoonekana wanavaa masuti na akili nyingi hawajasaidia lolote. Ni bora sisi twende na bukta bungeni lakini tuwe na vitu kichwani vya kuongea.”

Afande Sele aliongeza kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kuzingatia uandishi utakaoisadia jamii na pia watambue kuwa wasanii na wao ni watu wanaotakiwa kushirikiana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents