Habari

Madonna afungua kituo cha upasuaji Malawi

Mwanamuziki kutoka  nchini Marekani, Madonna amefungua taasisi itakayoweza kusaidia kufanya upasuaji wa watoto nchini Malawi.

Kituo hicho kimepewa jina la la mtoto wake wa Kike Mercy James Institute, lengo la kuanzishwa taasisi hiyo ni kuhakiksha watoto wa nchi hiyo wanapatiwa matibabu mazuri ili waweze kuwa na afya njema katika ukuaji wao.

Madonna ambaye amekuwa akiwaasili watoto amefanya uzinduzi wa kituo hicho Jumatatu ya wiki hii, kwa mujibu wa kituo cha CNN taasisi hiyo ni kituo cha kwanza kuanzishwa na mwanamama huyo ambaye alifika hapo mwaka 2006 kuanzisha kampeni yake ya “Raising Malawi” ili kusaidia watoto wenye matatizo.

Mwanamuziki huyo ameshawaasili watoto kama Mercy James kisha David Banda na baadae kuwaasili watoto mapacha Esther na Stella.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents