Habari
Mahakama ya mafisadi kuanza kutema cheche
Mahakama ya maalum ya ufisadi imeanza kufanya kazi zake.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Jaji mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othuman alisema mahakama hiyo imeanza kufanya kazi baada ya sheria yake kuwa tayari na kanuni zake kutolewa.
Alidai kuwa kesi kwenye mahakama hiyo zitachukua miezi tisa kusikilizwa na kutolewa hukumu.
Mahakama hiyo ilianzishwa kutokana na ahadi za Rais John Magufuli ambaye utawala wake umekuwa mstari wa mbele kupiga vita vitendo vya kifisadi.
BY: EMMY MWAIPOPO