Habari

Majaliwa awataka waislamu kuhubiri msingi wa dini hiyo

Waziri mkuu Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa waumini wa dini ya kiislamu nchini kutumia sehemu za ibada kuhubiri masuala ya Mungu na sio siasa .

rg1a0943

Waziri mkuu ametoa wito huo aliposhiriki sala ya Ijumaa katika msikiti wa Nunge mjini Dodoma na kuwataka waumini wa dini ya Kiislamu kutumia nyumba ya ibada kuhubiri msingi wa dini.

“Niendelee kusisitiza kwamba wote lazima tutumie muda wetu pamoja na mambo mengine lakini pia tumtafute Mungu kupitia nyumba za ibada. Ndugu waislamu wenzangu tufanye kazi ya kuujenga uislamu wetu kwa kuhakikisha kwamba nyumba hizi za dini kuhubiri uislamu,” alisema.

“Kuhubiri msingi wa dini lakini kusisitiza mshikamano miongoni mwetu kuhakikisha kwamba sisi na majirani zetu tunaishi kwa amani na utulivu, ni jukumu letu muhimu sana.”

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents