Burudani

Mambo mawili yanayompa furaha Beka Flavour  nje ya Yamoto Band

Baada ya kundi la Yamoto Band kutoa fursa kwa kila msanii wa kundi hilo kufanya kazi pekee yake (solo artist), msanii Beka Flavour ametaja mambo mawili ambayo anayafurahia wakati huu ambao anafanya muziki nje ya kundi.

Muimbaji huyo ambaye anatamba na wimbo ‘Libebe’ amekiambia kipindi cha Dj Show cha Radio One, kuwa mambo anayofurahia ni kuimba wimbo mzima pekee yake na uhuru wa kujiamulia mambo binafsi katika muziki.

“Vitu vingi vilikuwa vinanizuia, kwanza nilikuwa si-enjoy kwa sababu nilikuwa naimba verse fupi, mwenywe nilikuwa natamani niimbe verse ndefu lakini wenzio wataimba wapi, hicho ni kitu cha kwanza kilikuwa kinanibana,” amesema Beka Flavour.

Ameongeza “Kuna vitu vingi vimefunguka kupitia mimi mwenyewe, kwanza ilikuwa mtu akinihitaji ni lazima apitie kwa mtu mwingine na mwingine, au kuna kitu kingine ambacho mimi napenda kufanya zaidi ila uongozi unakuta unabana lakini sasa hivi vile navyopenda kuvifanya nafanya na uongozi upo.”

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents