Haji Manara baada ya Simba SC kutoka sare na Waarabu ‘heshima ya nchi imelindwa’
Baada ya klabu ya Simba jana Jumatano Machi 07, 2018 kutoka sare ya goli 2-2 na klabu ya Al-Masry kutoka nchini Misri, Msemaji wa klabu hiyo Haji Manara amewashukuru mashabiki wote waliojitokeza kushuhudia mchezo huo.
Manara amesema kuwa kitendo hicho ni cha mashabiki ni cha kiungwana na kizalendo pia kinaleta heshima kwa taifa letu.
“Kando ya Mwenyezimungu na wachezaji,hakuna anayestahili Shukran kama mashabiki mliokuja leo Taifa,mmetimiza wajibu wenu. Heshima ya nchi imelindwa🙏,“ameandika Manara kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii.
Soma na Hii – Mvua yawaokoa waarabu, Mnyama Simba SC atoka na uchu
Mchezo wa jana Simba walionesha kiwango cha kutia matumaini kwa Watanzania ingawaje mchezo huo ulitawaliwa na mvua kali iliyoambatana na radi.