Habari
Mike Tee kuingia kwenye siasa mwakani
Mnyalu Mike Tee ameamua kufuata nyayo za mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi kwa kutangaza nia ya kujihusisha na siasa.
Mike Tee ambaye siku za hivi karibuni amekuwa kimya kimuziki ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Facebook.
“Next year ni third phase of my life time. Naingia rasmi kwenye SIASA. Sijakurupuka nimefanya upembuzi akinifu for so long. Ntatumia muziki kuongea na jukwaa la siasa kuongea, kuna mambo mengi hayaendi sawa na watu wengi wanaogopa kuongea ukweli sababu ya watu wachache kubana.”
Hata hivyo amesema bado hajaamua chama atakachokuwa nacho bega kwa bega.