Burudani
Mke wa AY ajifungua mtoto wa kiume Marekani
Mke wa msanii mkongwe wa muziki wa hip hop, Ambwene Yessayah aka AY aitwaye, Remy siku ya jana amejifungua mtoto wa kwanza wa kiume huko Dallas -Texas nchini Marekani.
Jumatatu hii rapa huyo ameutaarifu umma kwamba mke wake huyo amepata mtoto wa kiume aitwaye Aviel ikiwa ni miezi 6 toka wawili hao waingie kwenye maisha ya ndoa.
“Mungu ni mwema na namshukuru sana kwa kutubariki mimi na My Beautiful Wife #Remy tarehe 12.08.2018 Medical City Healthcare Dallas -Texas tumepata mtoto wa kiume AVIEL maana yake GOD IS MY FATHER…. 3.9Kgs & 27 inches…Welcome to the World AVIEL YESSAYAH ππΏππΏππΏππΏππΏ,” aliandika rapa huyo kupitia instagram yake.
Mke wa rapa huyo ana asili ya Rwanda.
Huyo mtoto atakuwa raia wa uko uko Marekani, baba asili yake Tanzania, Mama asili ya Rwanda, inapendeza sana
Kumbe mama ilikuwa tayari.
Hongera zake
Nice kk
Huyo mtoto ni mmarekani
Hongera kwao
Money talks