Habari
Mmiliki wa mtando wa Facebook afuturisha wakimbizi
Mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook na CEO Mark Zuckerberg, amefuturisha wakimbizi wa nchini Somalia wanaoishi katika mji wa Minneapolis- Marekani.
Kupitia akaunti ya mtandao wa Instagram, Zuck alipost picha akiwa na baadhi ya wakimbizi hao wakati wa kula futari.
“I had my first Iftar dinner with a group of Somali refugees in Minneapolis. Thanks to my hosts for being so gracious at the very end of Ramadan,” ameandika Zuck.
Pia CEO huyo ameongeza kwa kuandika ” I left impressed by your strength and resilience to build a new life in an unfamiliar place, and you are a powerful reminder of why this country is so great.”
Na Laila Sued