Burudani
Mrisho Mpoto avuna nyanya za mamilioni, aeleza jinsi alivyopata hasara ya tsh milioni 60 kwenye kilimo (Video)
Msanii wa Muziki wa Asili, Mrisho Mpoto wiki hii amevuna nyanya zaidi ya tenga 250 ambazo zitampatia mamilioni ya pesa kutokana na kiungo hicho cha mboga kupotea sokoni na kugeuka dili ambapo kwa sasa nyanya moja unaizwa mpaka tsh 1000. Akieleza historia yake katika kilimo alipotembelewa na kamera ya Bongo5 akiwa shambani kwake, Mkuranga Mkoa wa Pwani, Mpoto alisema mara ya kwanza alikata tamaa kabisa kwenye kilimo baada ya kupata hasara ya zaidi ta milioni 60.