Burudani
Msanii wa dancehall wa Jamaica Vybz Kartel apatikana na hatia ya mauaji
Msanii wa dancehall wa nchini Jamaica, Vybz Kartel amepatikana na hatia ya mauaji. Yeye na watu wengine watatu walishikiliwa kwa kumuua Clive Lizard Williams.
Hukumu yao itatolewa March 27 huku mawakili wake msanii hiyo wakionesha dalili za kuikatia rufaa. Waendesha mashtaka walidai kuwa Williams alipigwa hadi kufa nyumbani kwa Kartel, 2011. Mwili wa mtu huyo haukuwahi kupatikana japo polisi wanadai kuwa waliwhai kukuta ujumbe kwenye simu ya Kartel unaodai kuwa Williams alisagwasagwa kiasi ambacho mabaki yake yasingepatikana.
http://www.youtube.com/watch?v=NYVvZiYDDr4
Kartel, ambaye jina lake halisi ni Adidja Palmer, ni miongoni mwa wasanii wakubwa zaidi nchini Jamaica.