Mtazame kwa ukaribu mtoto wa kike wa Fid Q, Fidelie
Fareed Kubanda aka Fid Q amemtambulisha kwa ukaribu binti yake mwenye mwezi mmoja sasa, Fidelie.
Mtoto huyo alizaliwa September 25 mwaka huu.
Rapper huyo amepost picha ya Fidelie kwenye Instagram na kuandika: #MalkiaWaNyamagana Bi #Fidelie.”
Hivi karibuni Fid Q alisema ni mapema kuzungumzia masuala ya ndoa na mpenzi wake kutoka Jamhuri ya Czech aliyemzalia mtoto huyo.
“Huyu ni mtoto wangu wa kwanza wa kike na kwa haraka haraka mimi nina watoto wawili wa kiume. Huyu mama yake alikuwa girlfriend wangu wa muda mrefu sana, yale masuala ya ndoa na nini nisingependa kuyaongelea leo, itakuwa umeyaharakisha sana lakini natarajia mambo mengi mazuri. Pia japokuwa nimetingwa na shughuli nyingi hapa nchini lakini nafanya mpango wa kukutana naye,” alisema Fid Q kwenye mahojiano na Clouds FM.