Mvua kubwa bado zitaendelea kunyesha – TMA
Maeneo mengine ni Pwani ya Kaskazini katika mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es Salaam, Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba.
Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya Hali ya Hewa wa TMA, Dk. Ladislaus Chang’a,amesema kuwa mvua hizo zimeendelea kupungua wakati zikifikia ukingoni.
“Mvua zinaendelea kupungua, lakini matukio machache ya mvua kubwa yanaweza kuwatokea, hivyo wananchi wanatakiwa kutufuatilia taarifa tunazotoa ili kuchukua tahadhari ingawa zimepungua lakini hatuwezi kusema zimeisha hadi msimu umalizike,” Alisema Dkt Chang’a kwenye mahojiano yake na Gazeti la Nipashe.
Aliendelea kusema katika maeneo hayo na yale ya kuzunguuka Ziwa Victoria wanapata mvua mara mbili kwa mwaka ambazo ni mvua za vuli na masika na kwamba kwa mwaka huu zilikuwa kubwa.
Alisisitiza kuwa msimu wa mvua kubwa bado unaendelea, ingawa zinaelekea ukingoni.