Burudani
Mwasiti adai ataendelea kukaa mbali na siasa
Mwasiti Almasi amedai kuwa yupo kuitumikia jamii zaidi na kazi zake za muziki na sio siasa.
Akiongea na E-News ya EATV, Mwasiti amedai kuwa pamoja na kuwa na uwezo mkubwa wa kuzungumza mambo ya msingi mbele ya watu, haoni kama muda wa yeye kuingia kwenye siasa umefika.
“Unajua sasa hivi sijafikiria kabisa kuingia katika siasa,” alisema.
“Roho yangu haijaniruhusu kwa sasa labda roho yangu ikiniruhusu baadaye sana sio mda wake sasa hivi japo nimekuwa muongeaji mzuri ninapokutana na vijana. Sasa hivi muda wangu mwingi ni kufanya mambo yangu.”