Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa ACT – Wazalendo wajidhamini wenyewe
Leo asubuhi Mwenyekiti wa Chama cha ACT – Wazalendo, Yeremiah Maganja, pamoja na Katibu Mkuu, Dorothy Semu, leo waliitikia wito wa Kamishna wa Makosa ya Jinai (DCI) wa Jeshi la Polisi katika kituo cha Polisi cha Kamata.
Mara baada ya mahojiano, viongozi hao wameachiwa kwa kujidhamini wenyewe na wanapaswa kurudi kituoni hapo jumatatu ya Novemba 27, mwaka huu.
Leo asubuhi Mwenyekiti wa Chama, ndugu Yeremiah Maganja, pamoja na Katibu Mkuu, ndugu Dorothy Semu, waliitikia wito wa Kamishna wa Makosa ya Jinai (DCI) wa Jeshi la Polisi katika kituo cha Polisi cha Kamata.
Mara baada ya mahojiano, viongozi hao waliachiwa kwa kujidhamini wenyewe na wanapaswa kurudi kituoni hapo jumatatu ya Novemba 27, 2017.
Taarifa zaidi juu ya yaliyojiri itatolewa baadaye.
Ado Shaibu – Katibu wa Itikadi, Mwasiliano ya Umma na Uenezi
ACT Wazalendo
Novemba 6, 2017
Soma zaidi: Wajumbe wa Kamati Kuu ACT – Wazalendo waitwa polisi kuhojiwa