Habari

Mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Kofi Annan umewasili Ghana kwa ajili ya maziko

Mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Kofi Annan umewasili Ghana kwa ajili ya maziko

Mwili wa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan, ambaye alifariki mwezi uliopita, umewasili katika nchi aliyozaliwa, Ghana.

Mwili wake uliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kotoka International Airport mjini Accra, ukisindikizwa na familia yake na maafisa wengine wa Umoja wa Mataifa

Kulikuwa na hali ya maombolezowakati mwili wake ukiwasili uwanjani hapo na kupokelewa na Rais wa Ghana Akufo Addo na viongozi wa kimila na kwa heshima ya kijeshi.

Mwili wake umehifadhiwa katika Ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Ghana, wakati ukisubiri kuzikwa.

DAVOS-KLOSTERS/SWITZERLAND, 30JAN09 – Kofi Annan, Secretary-General, United Nations (1997-2006); Member of the Foundation Board of the World Economic Forum; Co-Chair of the World Economic Forum Annual Meeting 2009, captured during the session ‘Fresh Solutions for Food Security’ at the Annual Meeting 2009 of the World Economic Forum in Davos, Switzerland, January 30, 2009.
Copyright by World Economic Forum swiss-image.ch/Photo by Sebastian Derungs

Kofi Annan alikuwa ni Katibu mkuu wa kwanza wa Umoja wa Mataifa, kutoka katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara na kuleta mafanikio sio tu katika bara la Afrika, lakini pia dunia nzima.

Chanzo BBC

By Ally Juma

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents