Habari
Mwizi alewa baada ya kuiba
Mwanaume mmoja nchini Australia ametiwa nguvuni na maafisa wa polisi baada ya kukutwa akiwa ameiba katika nyumba moja.
Mwanaume huyo mwenye miaka 36, alikutwa amelala kitandani baada ya kuiba na kisha kulewa katika nyumba hiyo iliyopo Esperence, magharibi mwa nchi hiyo.
Maafisa wa polisi wameeeleza kuwa walipigiwa simu na mwenye nyumba hiyo baada ya kumkuta muhalifu huyo akiwa amelala kitandani baada ya kulewa mvinyo.
Na Laila Sued