Habari

Naibu Waziri wa Mifugo Abdallah Ulega awatoa hofu wafugaji

Naibu waziri mifugo na uvuvi Abdallah Ulega (Aliyevalia shati la rangi ya njano) akizungumza na wafugaji mkoani Tanga.

Naibu Waziri wa Mifugo, Abdalah Ulega akizungumza na wafugaji

Serikali imewatoa  hofu wafugaji  nchini kuhusu  mchakato  wa  upigaji  chapa wa  mifugo  na kusema kuwa mpango huo haulengi kuchukua mifugo bali Serikali inataka kubaini  mifugo iliyopo.

Naibu Waziri  wa  Mifugo  na  Uvuvi, Abdallah  Ulega  ametoa hofu jana wakati akizungumza  na wakulima na wafugaji wa kijiji  cha  Perani  wilayani  Mkinga mkoa wa Tanga.

Kauli hiyo ya Ulega imekuja baada  wafugaji wa Perani kumweleza kwamba hawana elimu ya kutosha kuhusu mchakato huo na kwamba wanahisi kama mifugo yao inachukuliwa na Serikali .

Ulega  amesema Serikali ya Awamu ya Tano, ni sikivu na imedhamilia kuwatumikia vyema Watanzania na siyo kuwanyonya wananchi wa Taifa.

“Rais wetu ni mtu wa wanyonge, hakuna mtu yoyote atakayechukuliwa ngo’mbe zake.Bali tunataka  kujua mifugo yote iliyopo ili kuzuia mwingiliano na ile inayotoka nchi za jirani,”amesema  Ulega.

Naibu waziri huyo, ametumia nafasi hiyo kuwasihi wafugaji na wakulima wa  eneo hilo kuacha mapigano baina yao kwani siyo jambo zuli na halileti taswira nzuri

“Naomba muishi kwa amani na utulivu kuanzia leo tatizo lenu nitalifikisha ngazi ya juu kuanzia kwa mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigela  ili atume wataalamu waje kuangalia namna ya kusimamamia  vyema mpango kazi,”amesema Ulega.

Awali mwenyekiti wa kijiji hicho, Letinga Oyaya alimweleza naibu waziri huyo kwamba wanaomba kuelimishwa namna ambayo mchakato wa upigaji chapa utakavyotekelezwa na madhumuni yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents