Burudani

Napenda mwanaume anayeweza kuzungumza lugha nyingi na anayeijua historia za nchi mbalimbali – Rihanna

Ukitaka kuwa boyfriend wa Rihanna sharti ujipange!

1444683882_rihanna-article

Hii ni kwasababu mrembo huyo anataka kuwa na mwanaume anayejua vitu vingi sio ‘msingi kiuno’ kama wanaume wengi wa kibongo wanavyoamini!

“Navutia na wanaume wanaojua tamaduni. Hiyo itanifanya kushangazwa muda mwingi,” Rihanna ameliambia jarida la T.

“Sio lazima wawe na shahada yoyote, lakini wanatakiwa kuzungumza lugha zingine au kujua mambo kuhusu sehemu zingine za dunia au msanii ama mwanamuziki fulani. Napenda kufundishwa. Napenda kukaa kwenye upande huo mwingine wa meza.”

Hata hivyo Rihanna amesema kwa sasa hahitaji mwanaume kwakuwa akili yake ipo kwenye muziki na familia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents