Habari
Nimechoka kutoa rambirambi – Rais Magufuli (+video)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa amechoka kutuma salamu za rambirambi kufuatia ajali za barabararani zinazopoteza maisha ya wananchi bila Wizara ya Mambo ya Ndani kuchukua hatua, Kauli hiyo imekuja baada ya kutokea ajali mfululizo mkoani Mbeya bila wizara husika kutoa tamko lolote.