Burudani
Picha: Alikiba na Ne-Yo uso kwa uso jijini Nairobi
Muimbaji wa Mwana, Alikiba Jumatatu hii alikutana uso kwa uso na msanii wa Marekani, Ne-Yo kwenye kipindi cha Coke Studio Afrika jijini Nairobi, Kenya.
Alikiba na Ne-Yo walijumuika pia na wasanii wengine wa Afrika wakiwemo Wangechi (Kenya), Dama Do Bling (Mozambique), Ice Prince (Nigeria) na Maurice Kirya (Uganda).
Wasanii hao watarekodi wimbo wa pamoja. Msimu mpya wa Coke Studio Africa utazinduliwa Oktoba mwaka huu.