Picha: Mkutano wa Dkt. Mwakyembe na wasanii wa filamu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrion Mwakyembe leo Agosti 4, 2017 amekutana na wasanii wa filamu nchini katika ukumbi wa Mwl. Julius Nyerere Dar es Salaam ambapo wamejadili changamoto zinazoikumba tasnia hiyo kwa sasa.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe
Hapo jana Dkt. Mwakyembe alikutana na wasanii wa muziki na leo ikawa zamu ya wasanii wa filamu ambapo amewataka kutoiga vitu kutoka nje ya nchi huku akitolea mfano wingi wa makabila uliopo hapa nchini kuwa unaweza kutumika katika mambo mengi ya uigizaji.
Pia Dkt. Mwakyembe amewatakaa wasanii hao kubadilika ili kuendana na ukuaji wa teknolojia ili waweze kukuza kazi zao na kufika mbali zaidi ukilinganisha na sasa.
Tazama picha zaidi.
Bi. Joyce G.Fissoo Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzani
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba
Musa Sakari Mratibu wa sindano la European Youth Film Competition 2017 Andreson Media
Kikundi cha sanaa kutoka TaSUBa wakitoa igizo fupi
Picha ya pamoja ya Waziri na Viongozi na wasanii wa filamu
Na Laila Sued