Habari
Picha: Ushahidi kesi ya malkia wa meno ya tembo waendelea Kisutu Dar
Kesi inayomkabili raia wa China, Yang Feng Glan (66) maarufu kama Malkia wa tembo imeendelea tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam ambapo Ijumaa hii ushahidi juu ya kesi hiyo ukiendelea kutolewa.
Malkia wa meno ya tembo akiingia mahakamani
Kesi hiyo inasikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi chini ya wakili wa serikali Kishenyi Mutalemwa na wakili wa utetezi,Masumbuko Lamwai.
Mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake wawili anatuhumiwa kwa kufanya biashara ya vipande vya meno ya tembo 706 vyenye uzito wa kg 18892 thamani yake ikiwa ni shilingi bilioni 5.4 bila leseni ya Mkurugenzi wa wanyama pori.
Kesi hiyo itasikilizwa tena machi 14/15 mwezi ujao. Angalia picha.
By: Emmy Mwaipopo