Habari

Picha: Zanzibar yakumbwa na mafuriko, misaada ya kibinadamu inahitajika

Mafuriko makubwa yaliyosababishwa na mvua kali iliyonyesha kuanzia jana Jumapili na kuendelea hadi leo, yamesababisha maafa makubwa vikiwemo vifo na watu wengi kupotea makazi.

20150504105326
Eneo la uwanja wa ndege visiwani humo likiwa limejaa maji

Taarifa zinadai kuwa hadi sasa watu wawili wanadaiwa kupoteza maisha kutokana na mafuriko hayo. Nyumba nyingi zimejaa maji yaliyosababisha hasara kubwa.

dddd
Wananchi wakijaribu kuendelea na shughuli za kawaida licha ya maji kujaa hadi kufikia maeneo ya kiunoni

Akiongea na Bongo5, mmoja wa watu wanaounda timu inayoshughulikia masuala ya misaada ya kibinamu kwa waathirika, Arafat, amesema watu wengi wanahitaji misaada mbalimbali.

20150504105038
Barabara na miundombinu mingine imeathirika

“Jana ndio hali ilikuwa mbaya zaidi nyumba nyingi zilijaa maji zingine zilibomoka kutokana na nguvu ya mvua na wingi wa maji,” amesema.

20150504105039

Ameyataja maeneo yaliyoathirika zaidi na mafuriko ni pamoja na Kariakoo, Jang’ombe, Msendawe na Raha Leo. Arafat amedai kuwa pamoja na baadhi ya waathirika wa mafuriko kupewa hifadhi na ndugu zao, wapo waliokosa kabisa mahali pa kuishi hivyo wanafanya jitihada za kuwatafutia eneo moja la kuwahifadhi kwa muda.

20150504105056
Maji kwenye uwanja wa ndege yakiwa yamepungua baada ya kujaa

Ametaja mavazi, misaada ya vyakula, vifaa vya afya na madawa ndio vitu vinavyohitajika zaidi kwa sasa.
20150504105106

Kama umeguswa na unapenda kusaidia chochote, wasiliana na namba hizi. -0767278381 (Arafat) na Aysha- 0777888888.

Chini ni picha zingine za mafuriko hayo.

20150504105037

20150504105038

dar 2

dar 4

dar 5

dar 6

dar 7

dar 8

dar3

ddd

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents