Burudani
Producer Nash Designer kuachia wimbo mpya ‘Ndele’
Producer na mwandishi wa nyimbo, Nash Designer amesema anatarajia kuachia ngoma yake mpya iitwayo ‘Ndele’.
“Wimbo wangu wa Ndele nimeimba kutokana na misemo ambayo inazuka mitaani kwamba muziki sasa hivi umetawaliwa na waganga kwamba watu wana imani ukiloga basi unafanikiwa katika shughuli yako,” Nash ameiambia Bongo5.
“Kwahiyo ndio nikapata idea ya kuandika wimbo unaitwa “NDELE”. Maana ya ndele ni dawa ya asili ambayo inatumika kwa ajili mvuto katika kazi na kupendwa na watu tofauti kwa hiyo nikafikiria nataka wimbo uwe Wa tofauti ili uendane na idea nikaona iwe ya miondoka ya kiafrika.”