Habari
Rais Mstaafu Kikwete asajili laini yake kwa alama za vidole kabla ya tarehe ya mwisho
Rais wa Awamu ya 4, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo Januari 18, 2020 amesajili laini yake kwa njia ya kieletroniki, huku akiwahasa Watanzania wengine kujitokeza kushiriki zoezi hilo, kwa kuwa mwisho ni Januari 20, 2020.
Rais wa Awamu ya 4, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo Januari 18, 2020 akisajili laini yake kwa njia ya Kieletroniki
Rais wa Awamu ya 4, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo Januari 18, 2020 akisajili laini yake kwa njia ya Kieletroniki
Rais Mstaafu ameshiriki zoezi hilo leo ambapo amesema hatua ya kufanya hivyo ni kufuatia kuhimizwa na mfano aliouonesha Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya mwishoni mwa mwaka 2019.
Mpaka sasa bado siku 2 zoezi hili lifungwe.