Rapper Phyno amjibu aliyemwambia anavaa ‘Fake’
Rapper kutoka Nigeria, Phyno amemjibu kijana Hush Puppi ambaye alidai rapper huyo na msanii Ice Prince wanapendelea kuvaa vitu vilivyo fake.
Katika mahojiano aliyofanya na mtandao wa Punch, rapper amemjibu Hush Puppi kuwa haruhusiwi kuingilia maisha ya mtu na hamna mtu mwenye muda naye.
“It is very childish to brag about what I have..I care more about touching lives in positive ways. It is not really about how much you have in your bank account but how many people’s lives you have made better, amesema rapper huyo.
Ameongeza kuwa “The good thing is that I have a track record and people know what I do. So it doesn’t really make sense for me to be exchanging words with someone who just came from nowhere and has no credibility whatsoever.”
Hush Puppi ana umaarufu zaidi kupitia mitandao ya kijamii kutokana na kujinadi kuwa na pesa nyingi na anajua kuvaa.
Na Laila Sued