Mahojiano

Rayvanny: Diamond aliikataa verse yangu ya Quarantine, Amaboko ndio wimbo namba moja Afrika (+Video)

Msanii wa muziki kutokea kwenye lebo ya WCB @rayvanny siku ya leo aliamua kumfanyia suprise shabiki yake aliyechora picha yake kando kando ya barabara maeneo ya fire Posta jijini Dar Es Salaam.

Mbali na kukutana na kijana huyo pia walijitokeza mashabiki wengi kwa ajili ya kuonyesha love kwa @rayvanny

Bongo5 tulipata nafasi ya kupiga nae story na alizungumzia tukio hilo la picha yake kuchora kando kando mwa barabara.

Pia @rayvanny amezungumzia kuhusu ngoma mbili ambazo zimefanya vizuri sana ambazo ni Quarantine na Amaboko’ Vivan ameongeza kuwa Verse ya Quarantine Boss wake @diamondplatnumz hakuielewa kabisa hata rafiki zake walikuwa hawaitaki lakini cha kushangaza ndio moja ya verse pendwa kwenye ngoma hiyo. Kuhusu Amaboko ameeleza jinsi inavyofanya vizuri nje ya nchi na kuwashukuru mashabiki wake kwa kuendelea kumsapoti.

https://www.youtube.com/watch?v=Z7RtbEf6ibA

https://www.youtube.com/watch?v=T8hYoJ7LxZs

https://www.youtube.com/watch?v=zAJiS58gTdQ

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents