Habari

Rose Ndauka aitaka serikali kuongeza nguvu kusimamia kazi za wasanii

Msanii wa filamu nchini,Rose Ndauka ameitaka serikali kuongeza nguvu katika kusimamia kazi za wasanii.

13721319_1722856194642635_1471704036_n

Rose ametoa kauli hiyo alipokuwa akiuzungumzia utendaji wa Rais Magufuli katika kipindi cha mwaka mmoja toka achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kwenye tasnia ya filamu nikimuongelea Rais John Pombe Magufuli mi mabadiliko ninayoyafikiria ni mabadiliko zaidi ya haya ambayo tupo nayo sasa hivi. Mwaka mmoja wa Rais Magufuli serikali kuweza kusimamia kazi zetu vizuri, kuwe na muongozo mzuri kwenye upande wasanaa ili na wale producers au wale distributors waweze kujua kabisa sheria ziwe wazi,”Rose aliiambia TBC.

Rais Magufuli ametimiza mwaka mmoja tangu aingine madarakani hivyo watu mbalimbali wamekuwa wakiuzungumzia utendaji kazi wake.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents