Habari

Serikali yasitisha ujenzi wa barabara ya Makongo kuelekea Goba

Serikali imesema imesitisha mpango wa kujenga barabara inayotoka Makongo kuelekea Goba na mkandarasi kuondoka katika  eneo hilo kutokana na hali ya mvua inayoendelea kunyesha katika maeneo mengi hapa nchini.

Akijibu swali la mbunge wa Kawe Mhe.Halima Mdee aliyeuliza ni lini serikali barabara inayotoka chuo cha ardhi kwenda Makongo hadi Goba itajengwa kwa kiwango cha lami na wananchi kulipwa fidia.

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilianao Mhe.Isack Kamwelwe amekiri kuwa mkandarasi ameondoka katika eneo hilo kutokana na mvua zinazoendelea na kusisitiza kitaalamu kuwa barabara haziwezi kutengenezwa msimu wa mvua kutokana na hali ya udongo.

Source: ITV

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents