Habari
Shirika la ndege la Israel, Al Israel Airlines kuzindua safari zake za Tanzania mwezi April
Mwezi April, Tanzania itapokea watalii wengi kutoka Israel, pale shirika lenye makazi yake jijini Tel Aviv la El Al Israel Airlines litakapoanzisha safari za mara moja kwa wiki kwenye uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro, KIA.
Takriban watalii 150 kutoka Israel watakuwa wakija Tanzania kila wiki na hivyo kuleta watalii 600 Israeli kila mwezi.
Wengi wa watalii hao watakuwa wakija kwaajili ya kupata Mlima Kilimanjaro, Ngorongoro Crater, Mbuga ya wanyama ya Serengeti, Hifadhi ya taifa ya Tarangire, Arusha na ziwa Manyara.