Habari
Steps Entertainment yaja na tuzo ‘kimya kimya’ Bongo Movie Awards 2012 – 2013 zitakazotolewa June 15
Kampuni ya utayarishaji na usambazaji wa filamu nchini, Steps Entertainment imeandaa tuzo ziitwazo ‘Bongo Movie Awards 2012 – 2013’ zitakazotolewa June 15 kwenye ukumbi wa Blue Pearl Hotel – Ubungo.
Tuzo hizo zimekuja kimya kimya kwakuwa hakuna mchakato wowote uliotangazwa kuhusu tuzo hizo hadi leo ambapo wametangaza tarehe ya kutolewa kwake.
Tumejaribu kuongea na uongozi wa Steps kuhusu tuzo hizo lakini wamedai watatoa taarifa baadaye.
Inaonekana tuzo hizo zitahusisha filamu zinazoandaliwa na kusambazwa na kampuni hiyo tu.