Habari

Uchaguzi Kenya: Baba mzazi wa Lupita Nyongo anyakua jimbo

Baba mzazi wa mugizaji kutoka Kenya, Lupita Nyongo, Professor Anyanga Nyongo amefanikiwa kunyakua kiti za ugavana katika jimbo la Kisumu nchini Kenya.

Katika uchaguzi huo Prof. Nyongo amepata kura takriban 252,490 sawa na asilimia 63 huku wapinzani wake Jackson Ramguma akipata kura 141,320 ambazo ni sawa na 36% na Christine Otieno akipata kura 1919 sawa na 1% ya kura zilizopigwa katika jimbo hilo.

Katika jimbo hilo la Kisumu mgombea kutoka National Super Alliance (NASA), Raila Odinga amepata kura 6,164,403 sawa na 44.58%, wakati rais Uhuru Kenyatta amepata kura 7,546,262 sawa na 54.57%.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents