Michezo
UEFAChampionsLeague: Lukaku, Fellaini waibeba Manchester United (+Video)
Klabu ya Manchester United imeanza safari yake ya kupigania ubingwa wa kombe la klabu bingwa barani Ulaya vizuri kwa kuitwanga klabu ya FC Basel goli 3-0.
https://youtu.be/zcqD7k8YAl8
Magoli ya Manchester United yametupiwa ‘Manywele’ Maroune Fellaini, Romelu Lukaku na Rashford na kuifanya klabu hiyo kuongoza katika kundi A linaloundwa na klabu ya CSK Moscow na Benfica ya Ureno.
Matokeo mengine kwenye kundi hilo ni kwamba, CSKA Moscow wamechomoza na ushindi wa ugenini wa goli 2-1 dhidi ya Benfica.