Burudani
Usher kuigiza kama bondia Sugar Ray kwenye filamu mpya
Muimbaji wa R&B wa Marekani, Usher ataigiza kama bondia Sugar Ray Leonard kwenye filamu mpya iitwayo ‘Hands of Stone’.
Muimbaji huyo wa ‘Scream’ amesema amefurahia kushiriki kwenye filamu hiyo kwakuwa amejifunza kupigana na kuboresha mwili wake.
Akiongea kwenye kipindi cha ‘Live with Kelly and Michael’, alisema: “Nimekuwa nikifanyia kazi kwa mwaka mmoja sasa na tumeimaliza. Ni nzuri sana. Nilijifunza kama bondia, sasa hivi nipo vizuri kwenye mikono yangu.”