Habari
Video: Kontena za Makonda kaa la moto, hata moja halijauzika katika mnada wa leo
Makontena yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, yameshindwa kuuzwa Jumamosi hii baada ya wateja ambao walikuwa mnadani hapo kushindwa kufika bei. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefikia hatua ya kupiga mnada kontena hizo baada ya kudai kodi ya Tsh bilioni 1.2.