Burudani
Video: Ray C aonjesha nyimbo zake mbili mpya
Rehema Chalamila aka Ray C, yupo studio ambako anaendelea kurekodi nyimbo mpya. Muimbaji huyo mwenye sauti tamu na aliyekuwa akisifika kwa kiuno chake kisichokuwa na mfupa, ameshare video kwenye mtandao wa Instagram wa nyimbo zake mpya.
Moja ya video hiyo unasikika wimbo wake wenye mahadhi kama ya taarab huku akiimba ‘binadamu ni wabaya, sura zao hazina haya, mambo yanatunyookea, issue zetu ziko sawa’.
Na video nyingine inamuonesha Muki, wa kundi la Makomando akicheza wimbo uliochangamka kiasi unaonekana ameshirikishwa na Ray C.
Unadhani nyimbo hizo zinaweza kumrudisha kwenye chart?