Michezo

Wachezaji wawili wa Manchester wafukuzwa kambi ya timu ya taifa kisa kupeleka wanawake kambini (+Video)

Wachezaji wawili wa tim ya taifa ya Uingereza Maso Greenwood pamoja na Phil Foden tayari wamefukuzwa  kutoka kwenye kikosi cha Gareth Southgate, lakini huenda hivi karibuni wakapata adhabu kali zaidi.


Phil Foden na Mason Greenwood watakabiliwa na faini baada ya uthibitisho kutoka kwa polisi nchini Iceland kwamba uchunguzi kufanyika juu ya ukiukaji wa itifaki ya kukaa kambini na kufuata sheria dhidi ya Corona.

Foden na Greenwood wote waliondolewa kwenye kikosi cha hivi karibuni cha Uingereza Jumatatu ambacho kitaenda kukabiliana na Denmark kufuatia madai kwamba walialika wasichana kwenda kwenye hoteli ya timu huko Reykjavik, Iceland.

Wachezaji hao wote watarudishwa England pia watalazimika kufuata miongozo ya karantini kabla ya kurudi kwenye  vilabu vyao ambavyo ni Manchester City na Manchester United.

Gareth Southgate alithibitisha kuwa wawili hao walikuwa wamevunja sheria za kujikinga na Covid-19 kwenye mkutano na waandishi wa habari kabla ya pambano la timu yake na Denmark ambalo litachezwa leo Jumanne.

“Hawa ni wavulana wawili ambao siwajui vizuri kwa sasa kwa hivyo hawawezi kuzungumza kwa kina sana,” alisema bosi huyo wa England. “Lazima nijaribu na kuzungumza nao baadaye kwa njia inayofaa.

“Wana majukumu na wameomba msamaha. Kilicho wazi ni kwamba kulikuwa na ukiukaji wa miongozo ya coronavirus. Tulitumia muda mrefu kupata hatua hizo  na kikosi kizima kilifuata hiyo pamoja.

“Siwezi kusema tatizo ni umri wao na hueda ikawa tatizo ni makuzi ila Wameonyesha tabia mbaya sana Ni wazi, wamekuwa wajinga, tumewashughulikia ipasavyo.”

Afisa wa vyombo vya habari wa polisi Gunnar Sveinbjornsson aliiambia Telegraph: “Imeletwa kwetu na tutaiangalia. Lakini ni mapema mno, nam ipo wazi, kusema matokeo yatakuwa nini. ”

Sveinbjornsson aliendelea kuongeza kuwa ukiukaji wa sheria za coronavirus za nchi hiyo huwa inatolewa adhabu lakini lazima faini itoke pia”.

Foden na Greenwood wote wawili walipewa nafasi ya kucheza na timu ya taifa wakati wa ushindi wa 1-0 wa England dhidi ya Iceland Jumamosi jioni, ambapo  winga wa City Raheem Sterling alifunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penati.

Mason Greenwood wa Manchester United ana umri wa miaka 18 huku Phil Foden wa Manchester Citry akiwa na miaka 20.

https://www.instagram.com/tv/CE3ezo9DcDB/

https://www.youtube.com/watch?v=–8_K8i_n90

https://www.youtube.com/watch?v=mkdIZEWJvrY

https://www.youtube.com/watch?v=RqlNWL0C0rE

https://www.youtube.com/watch?v=lgMjkpAamsQ

https://www.youtube.com/watch?v=HwctESjdeFE

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents