Wafungwa 35 wauawa kikatili Gerezani
Gavana wa jimbo la Amazonas nchini Venezuela, Liborio Guarulla amesema zaidi ya wafungwa 35 wameuawa kwa kupigwa risasi gerezani katika kile kilichoitwa ‘Mauaji kwa watumiaji madawa’ kinachotekelezwa na maaskari nchini humo.
Kikosi maalumu cha jeshi cha wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo leo Agosti 17 kimepelekwa kudhibiti hali ya ndani ya gereza katika mji mkuu wa jimbo hilo, Puerto Ayacucho.
Masacre en el Centro de Reclusión ( CEDJA) de Pto Ayacucho, más de 35 cadaveres dejó la toma de este centro por la Unidad Especial del MRIJP
— Liborio Guarulla (@LiborioGuarulla) August 16, 2017
Taarifa kutoka shirika la habari la AFP zinaeleza kuwa Watu waliokaribu na gereza hilo walishuhudia tukio hilo kwa kusema walisikia milio ya risasi kwa saa kadhaa na vilio, ingawaje mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Serikali.
Asasi nyingi za kiraia nchini humo na zile za kimataifa zimekuwa zikilaumu uongozi wa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwa kutokuzingatia haki za binadamu baada ya kutekeleza mauaji dhidi ya watu wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya ikiwemo wafungwa ambao walihukumiwa kwa makosa kama hayo.