Habari

Wasiosajili majina ya biashara wapewa siku 60 kusajili kuepuka msako

Wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA),Frank Kanyusi, ametoa muda wa siku 60 kwa wafanyabiashara wanaotumia majina ya biashara pasipo kusajiliwa, na kuamuru wafanye hivyo haraka.

frank-kanyusi

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kanyusi alisema katika kazi hiyo ya kutoa elimu na kurasimisha majina ya biashara na kampuni inayoendelea katika mikoa mbalimbali, imebainika kuwa wafanyabiashara wengi wanatumia majina ya biashara pasipo kuyasajili.

“Natoa kipindi cha siku 60 kuanzia leo kila mfanyabiashara ahakikishe ana sajili jina lake la biashara, baada ya hapo nitafanya msako nchi nzima kukagua majina ya biashara, ili kubaini yale majina ambayo hayajasajiliwa,” alisema Kanyusi.

Aidha Kanyusi alisema usajili wa majina ya biashara umerahisishwa na wafanya biashara wanaweza kusajili jina la biashara yake kwa njia ya mtandao.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents