Habari

Waziri Lugola atinga Wizarani afanya kikao na watendaji wakuu (+Picha)

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola leo amewasili Wizarani na kupokelewa Ofisi ndogo za Wizara hiyo zilizopo jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Kangi Lugola, akiongozana na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), baada ya kupokelewa leo ofisi ndogo ya wizara,jijini Dar es Salaam

Tazama picha zaidi:

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na viongozi wengine wa wizara hiyo akiwepo Naibu Waziri, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto),Katibu Mkuu, Meja Jenerali Jacob Kingu (wapili kulia), Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima(wakwanza kulia).Wakwanza kushoto ni aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo,Balozi Hassan Simba Yahaya.Kikao hicho kimefanyika leo,jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa kikao cha viongozi wakuu wa wizara hiyo,Waziri Kangi Lugola(watatu kulia), Katibu Mkuu, Meja Jenerali Jacob Kingu (wapili kulia), Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima(wakwanza kulia),aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo,Balozi Hassan Simba Yahaya(wapili kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili wa Vyama vya Kijamii, Marlin Komba(wakwanza kushoto).Kikao hicho kimefanyika leo,jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Kangi Lugola,akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, baada ya kufika Ofisi ndogo ya wizara jijini, Dar es Salaam leo


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akisalimiana na Maafisa wa Jeshi baada ya kufika Ofisi Ndogo ya wizara,jijini Dar es Salaam, leo.

Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents