Burudani
Young Killer kuachia ngoma mpya ‘My Power’ wiki ijayo
Rapper wa Mwanza. Young Killer amesema wiki wiki ijayo anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa, My Power.
Amesema tangu atoe video ya Mrs Supastaa, amepokea maoni mengi yaliyomtia moyo.
“Unajua kila kitu cha mafanikio kwenye maisha yako ni hatua muhimu sana,maoni mazuri ya watu mbalimbali na wadau wa muziki yamenipa matumaini ya kile ninachokifanya katika maisha ya muziki wangu,” ameiambia Bongo5. Kwahiyo bila kuwacheleweshea wiki ijayo naachia wimbo wangu mpya ‘My Power’, kwenye video watu waendelee kuangalia Mr Super Star na kwenye redio wapate wimbo mpya My Power.”