Zimbabwe hali si shwari, Jeshi lazingira kituo cha utangazaji cha taifa
Jeshi la Zimbabwe limezingira kituo cha utangazaji cha taifa nchini humo, (ZBC) likidai kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu na kurudisha amani nchini humo.
#Zimbabwe is waking up to a new reality as the Army takes control of the country. What next as order as #RobertMugabe has been put under the army’s ‘care’ Apparently a number of ministers are facing arrest. #sabcnews pic.twitter.com/nfSDY1FZZz
— Peter Ndoro (@peterndoro) November 15, 2017
Jeshi hilo linasema kuwa hayo sio mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Rais Mugabe kama wengi wanavyodhani kwani Rais Mugabe bado yupo madarakani na yuko salama.
Baada ya tukio hilo la wanajeshi kuzingira na kudhibiti kituo hicho cha habari, imeripotiwa kuwa asubuhi ya kuamkia leo milio ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Harare.
Kwa mujibu wa maelezo kutoka katika gazeti la News 24 linadai kuwa moja ya viongozi wa jeshi hilo ambaye hakutaka kujitambulisha amesema jeshi hilo linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.
Mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Rais Mugabe na hakuna mfanyakazi wa Shirika hilo la utangazaji aliyejeruhiwa kwenye ufamizi huo wa majeshi.
Hali ya usalama nchini Zimbabwe imekuwa tete tangu Rais Mugabe amtoe madarakani aliyekuwa makamu wake wa Rais, Emmerson Mnangagwa.
SOMA ZAIDI-Rais Mugabe amtumbua Makamu wake wa Rais
Tayari ofisi zote za kiserikali nchini humo zimefungwa ikiwemo ubalozi wa Marekani nchini humo ambao kupitia ukurasa wao wa Twitter umetangaza kuwa leo hautafungua ofisi zake mpaka hali itakapotengamaa.
Due to ongoing uncertainty in Zimbabwe, the U.S. Embassy in Harare will be minimally staffed and closed to the public on November 15. Embassy personnel will continue to monitor the situation closely. @StateDept
— U.S. Embassy Zimbabwe (@USEmbZim) November 15, 2017