Michezo
Ligi Kuu yapata mdhamini rasmi, TFF yalamba mamilioni Rais Karia atoa onyo kali ”Ole wake klabu iombe tubadili ratiba” (+Video)
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom wamesaini Mkataba wa miaka 3 wa Udhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Mkataba huo unathamani ya shilingi bilioni 9 ambapo kila mwaka shilingi bilioni 3.
Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, Wallace Karia ”Changamoto moja wapo ni ratiba, tunaomba viongozi wa vilabu waheshimu ratiba, asije kiongozi akaja kutakata ratiba irekebishwe na nyinyi waandishi wa habari mkampa sapoti. Mwaka huu tupo makini hatutakuwa tayari kubadili ratiba labda inyeshe mvua ya mawe, hatutakuwa na mchezo kwenye ratiba.”