Rais Samia Suluhu Hassan akiwa miongoni mwa baadhi ya wakuu wa nchi ndani ya basi wakielekea katika eneo la Westminster Abbey jijini London ambapo yatafanyika mazishi ya Malkia Elizabeth II.
Wengine waliokuwa kwenye basi hilo ni Rais wa Kenya, William Ruto na mkewe Rachel na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mbarouk Nassor Mbarouk.
Mazishi hayo yanafanyika leo na kuhudhuriwa na zaidi ya watu 2,000 wakiwamo viongozi 500 wa nchi, serikali, taasisi na mashirika mbalimbali ya kimataifa duniani.