Katika usiku wa ijumaa ya 3 juni, bendi saba za taarab zitaungana pamoja kwaajiri ya tamasha la pamoja pale New Msasani ili kuchangia fedha za uzazi salama kwa kina mama.Katika tamasha hilo ambalo litapambwa na waimbaji maarufu kamaMwanahawa, Khadija Kopa, Omary Tego, Naima Mauwa Tego, Queen Salma, Mariam, Hammer Q , Sikudhani na Hashim Saidi, linakuwa la kipekee kutokana na makundi hayo kuweka tofauti zao kwa siku hiyo.
Aidha anasema kiongozi wa QSSP group ambao ndiyo waendeshaji wa tamasha hilo, wamesema bendi ambazo kwa siku hiyo zitapanda jukwani ikiwemo East African Melody, TOT Taarab, New Zanzibar Stars, Coast Modern Taarab, Dar Modern Taarab, Super Shine Modern taarab na Eagle Modern Taarab.