Michezo
Andy Murray atupwa nje ya mashindano ya US Open
Mcheza tenesi namba mbili duniani Muingereza, Andy Murray ametolewa katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya US Open baada kupokea kichapo cha seti 1-6,6-4,4-6,6-1,7-5 kutoka kwa Mjapan Kei Nishikori.
Nishikori ambaye ni mchezaji namba 6 kwa ubora duniani, atachuana na Stan Wawrinka aliyemshinda Juan Martin del Potro kwa seti 7-6 4-6 6-3 6-2.