Burudani
Nick Young anatamani ex wake, Iggy Azalea aolewe na French Montana
Aliyekuwa mpenzi wa Iggy Azalea, Nick Young amesema kuwa anaamini ex wake huyo ataolewa na French Montana ambaye ni mpenzi wake mpya.
Nick Young ameuambia mtandao wa TMZ kuwa anafurahi kuwaona wawili hao wakiwa pamoja. “No man, I’m happy for them. I wish they’d get married,” amesema Nick.
Iggy aliwahi kutaja sababu ya kuachana na Nick kuwa kutokana na kugundua kuwa ex wake huyo ana mahusiano na wanawake wengine wa nje.
Kwa sasa Iggy yupo kwenye mahusiano na French Montana kwa zaidi ya mwezi mmoja kutokana na matukio yao yanayoonekana mitandaoni wakiwa pamoja sehemu mbalimbali za starehe japo hakuna kati yao aliyethibitisha.